Kabul: Inadaiwa helikopta ya Kimarekani imedunguliwa huko Afghanistan
18 Februari 2007Matangazo
Majeshi ya muungano yanayoongozwa na Marekani katika Afghanistan yamesema moja ya helikopta zao imeanguka katika eneo la kusini mashariki ya nchi hiyo. Katika taarifa, muungano huo umesema ulianzisha msako na shughuli ya kuiokoa helikopa hiyo na watu waliokuwemo ndani yake baada ya rubani kuripoti kwamba aligundua kuna hitilafu katika injini ya helikopta hiyo. Waasi wa Taliban wanadai wameidungua helikopta hiyo kwa kutumia roketi.