KABUL: Mashambulio yameua raia Afghanistan
10 Mei 2007Matangazo
Raia 21 wameuawa katika shambulio la angani nchini Afghanistan.Gavana wa mkoa wa Helmand kusini mwa nchi amesema,wanawake na watoto ni miongoni mwa wale waliouawa.Kwa upande mwingine maafisa wa kijeshi wa Marekani wamesema mwanajeshi wao mmoja aliuawa katika mapigano na waasi wa Kitaliban katika wilaya ya Sangin huko Helmand.Wakati huo huo wakasema kuwa wao hawana habari yo yote kuhusu vifo vya raia.