Kabul. Mripuko wauaa watu 28.
2 Mei 2005Matangazo
Watu 29 wameuawa baada ya bohari la silaha kuripuka kaskazini mwa Afghanistan.
Taarifa iliyotolewa na serikali pia imefahamisha kwamba watu wengine sabini wamejeruhiwa.
Msemaji wa wizara ya ndani ya Afghanistan bwana Lutfullah Mashal ameeleza kwamba eneo lote la karibu ya bohari hilo limeteketezwa.
Kuna hofu kwamba wanawake na watoto ni miongoni mwa wahanga wa ajali hiyo.
Uchunguzi juu ya ajali hiyo unafanyika.