1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kabul. Mwandishi aachiwa huru.

20 Machi 2007

Mwandishi habari raia wa Italia ambaye alikuwa akishikiliwa mateka kwa muda wa wiki mbili na wapiganaji wa Taliban nchini Afghanistan ameachiliwa huru.

Waziri mkuu wa Italia Romano Prodi amethibitisha kuwa Daniele Mastrogiacomo alikuwa katika hali nzuri na alikuwa anapatiwa matibabu katika hospitali inayoendeshwa na Wataliani katika jimbo la Helmand.

Mastrogiacomo alikamatwa karibu na eneo hilo mapema mwezi huu wakati alipokuwa akisafiri kwenda kukutana na kamanda wa Taliban.

Wapiganaji hao walitishia kumuua Mastrogiacomo hadi pale viongozi watatu wa Taliban walioko jela watakapoachiliwa na serikali ya Afghanistan.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW