1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KABUL: Washukiwa saba wa al-Qaeda wauwawa

24 Agosti 2006

Wanajeshi wa Marekani na wa Afghanistan wamewaua washukiwa saba wa kundi la al-Qaeda mashariki mwa Afghanistan.

Jeshi la Marekani limesema lilifanya operesheni ya kumsaka na kumkamata mwanaharakati wa al-Qaeda kwenye kijiji cha Asmar katika mkoa wa Kunar.

Lakini maofisa wa Afghanistan kwa upande wao wamesema watu wote saba waliouwawa ni raia.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW