1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kallas: EU kuchukua "hatua muhimu" wiki hii kuhusu Ukraine

15 Desemba 2025

Viongozi wa Umoja wa Ulaya wanatarajiwa katika mkutano wa kilele wiki hii, kuchukua hatua muhimu kuhusu ufadhili wa kuisaidia Ukraine, lakini mazungumzo kuhusu kutumia mali za Urusi zilizozuiwa yanazidi kuwa magumu.

Brussels I Mwanadiplomasia Mkuu Umoja wa Ulaya Kaja Kallas
Mwanadiplomasia Mkuu Umoja wa Ulaya Kaja Kallas akizungumza mjini BrusselsPicha: Nicolas Tucat/AFP

Hayo yamesemwa Jumatatu na mwanadiplomasia mkuu Umoja wa Ulaya Kaja Kallas aliyesisitiza kuwa hilo linaendelea kujadiliwa:

"Kwanza kuhusu suala la kuifadhili Ukraine tunayo wiki ya kulijadili hilo kwa kina. Mada hizi na maamuzi tunayopaswa kufanya ili kuiunga mkono Ukraine, nadhani ni muhimu sana."

Viongozi 27 wa Umoja wa Ulaya watakutana mjini Brussels siku ya Alhamisi kujaribu kufanikisha mpango huo wa kuifadhili Kyiv kwa miaka ijayo. Hata hivyo Ubelgiji inayohifadhi mali zaidi za Urusi zilizozuiwa, inapinga mpango wa kutumia fedha hizo zipatazo dola bilioni 106 kama mkopo wa kufidia uharibifu uliotokana na vita vya Urusi nchini Ukraine . Ubelgiji inataka hakikisho la mataifa yote ya Ulaya kushirikiana kulipa fedha hizo ikiwa itahitajika hapo baadaye.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW