Kamerun na Misri kupambana fainali
8 Februari 2008Matangazo
KUMASI:
Katika fainali ya kuwania Kombe la Afrika,Misri inayotetea ubingwa wake itapambana na Kamerun siku ya Jumapili mjini Accra.Katika nusu fainali iliyochezwa siku ya Alkhamisi mjini Kumasi,Misri iliipachika Ivory Coast mabao 4-1.
Wakati huo huo Kamerun imejipatia tikti ya kuingia katika fainali baada ya kuwakandika wenyeji Ghana bao 1-0.