Merz awasili China kwa mazungumzo ya biashara na usalama
25 Februari 2026
Matangazo
Katika mazungumzo yake na Waziri Mkuu wa China Li Qiang mara baada ya kuwasili Beijing, Merz amesema anazingatia umuhimu mkubwa katika kuimarisha zaidi ushirikiano kkadri iwezekanavyo.
Ziara ya kwanza China tangu Merz alipoingia madarakani
Ziara hii ni ya kwanza ya Merz katika taifa hilo ambalo ni mshirika mkubwa wa kibiashara kwa Ujerumani. China pia ni mshindani mkubwa wa kiteknolojia kwa Ujerumani iliyo na uchumi mkubwa zaidi barani Ulaya.
Katika mazungumzo yake atakayofanya na Rais Xi Jinping, Merz anatarajiwa kutilia mkazo maslahi ya Ujerumani na Ulaya, ikiwemo kuongeza shinikizo kwa Urusi kumaliza vita nchini Ukraine.