1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Stoltenberg: Bajeti ya kijeshi imeongezeka kwa 11%

14 Februari 2024

Katibu Mkuu wa mfungamano wa kijeshi wa NATO Jens Stoltenberg, amesema bajeti ya kijeshi ya mfungamano huo imeongezeka mwaka uliopita na kufikia 11% kwa nchi wanachama ikiwa pamoja na Canada na washirika wake wa Ulaya.

NATO | Jens Stoltenberg
Katibu Mkuu wa NATO Jens StoltenbergPicha: John Thys/AFP

Stoltenberg amesema anatarajia wanachama 18 watatenga asilimia 2 ya mapato jumla ya nchi zao hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu.

Katibu Mkuu wa mfungamano wa kijeshi wa NATO ameeleza kuwa hilo ni ongezeko la mara sita zaidi kuliko ilivyokuwa mnamo mwaka 2014 ambapo ni nchi tatu tu wanachama zilizofikia kiwango hicho.

Soma pia:Ujerumani yafikia lengo la NATO katika kujilinda

Mnamo mwaka 2006 nchi wanachama wa NATO zilikubaliana kutenga asilimia 2 ya pato jumla kwa ajili ya ulinzi lakini ni nchi chache tu zilizofikia lengo hilo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW