1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Katibu Mkuu wa NATO kukutana na Trump mjini Washington

8 Aprili 2026

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO Mark Rutte yuko mjini Washington na anatarajiwa Jumatano kukutana na Rais wa Marekani Donald Trump kujaribu kutuliza ghadhabu ya Trump dhidi ya muungano huo wa kijeshi.

Katibu Mkuu wa NATO Mark Rutte akiwa na rais Donald Trump
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO Mark Rutte akizungumza na Rais wa Marekani Donald TrumpPicha: Mandel Ngan/AFP/Getty Images

Trump ambaye amekuwa akiwatuhumu washirika wa Ulaya kwa kushindwa kusaidia kuufungua Mlango-Bahari wa Hormuz uliofungwa kutokana na vita vya Iran, ametishia mara kadhaa kuiondoa Marekani kwenye jumuiya ya NATO.

Viongozi hao wawili wanatarajiwa kuzungumza kuhusu mzozo wa Ukraine na Mashariki ya Kati. Ikulu ya White House imesema mkutano huo umepangwa kufanyika faraghani lakini huenda hilo likabadilika mnamo dakika za mwisho na hivyo kuwaruhusu waandishi wa habari kuhudhuria.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW