Katibu Mkuu wa NATO kufanya ziara ya siku mbili Marekani
13 Julai 2025
Matangazo
Hayo yameelezwa kupitia taarifa iliyotolewa Jumapili japo haikufafanua madhumuni ya ziara ya Rutte itakayoanza Jumatatu 14.07.2025 nchini Marekani. Hata hiyo hivi karibuni Trump alisema katika mahojiano na kituo cha habari cha NBC kwamba Marekani itakuwa tayari kuipatia silaha Ukraine kupitia Jumuiya ya kujihami ya NATO na kwamba angelitoa "taarifa muhimu" kuhusu Urusi Jumatatu.
Utawala wa Trump umekuwa ukituma silaha zilizoidhinishwa na mtangulizi wake Joe Biden, aliyeiunga mkono kikamilifu Kyiv. Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amekuwa akiwatolewa wito washirika wake wa Magharibi kuipatia silaha zaidi ili kukabiliana na mashambulizi ya Urusi yanayoongezeka.