SiasaIraq
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guteress yuko Irak
1 Machi 2023![Schweiz, Genf | António Guterres im UN-Menschenrechtsrat](https://static.dw.com/image/64829168_800.webp)
Matangazo
Ziara hiyo ya Guterres ambayo ni yake ya kwanza nchini humo katika kipindi cha miaka sita, inakuja wakati ambapo nchi hiyo inayokabiliwa na vita inajiandaa kuadhimisha miaka 20 tangu kuondolewa madarakani kwa dikteta wa muda mrefu Saddam Hussein, katika operesheni iliyoongozwa na Marekani.
Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa amesma anataka kuonyesha mshikamano na watu na taasisi za kidemokrasia za Irak na mshikamano unaomaanisha Umoja wa Mataifa umedhamiria kikamilifu kuunga mkono uimarishaji wa taasisi za nchi hiyo.