1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Keita aunda serikali mpya kukabili mkwamo wa kisiasa Mali

Daniel Gakuba
28 Julai 2020

Rais Ibrahim Boubakar Keita wa Mali ameunda baraza dogo lenye mawaziri sita lililotwishwa jukumu la kutafuta suluhu kwa mgogoro wa kisiasa unaoendelea kuighubika nchi hiyo, huku akitakiwa pia kuvunja bunge.

Mali Präsident Mahamadou IssoufouI aus Nigeria von Präsident Ibrahim Boubacar Keïta begrüßt
Picha: Présidence du Mali

Keita ambaye tangu mwezi Aprili amekuwa hana baraza la mawaziri, ameliunda baraza hilo chini ya shinikizo la Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi, ECOWAS, ambayo imehusika katika juhudi za kutanzua mzozo wa nchi yake.

Mawaziri watatu wamerejea katika nyadhifa zao za awali, ambao ni Waziri wa Ulinzi Ibrahima Dahirou Dembele, Waziri wa Utawala wa Kimajimbo Boubacar Alpha Bah na Waziri wa Mambo ya Kigeni Tiebile Drame.

Wapya walioingia ni Kassoum Tapo aliyeteuliwa kuwa waziri wa sheria, Abdoulaye Daffe aliyewekwa katika wizara ya fedha, na Bemba Moussa Keita ambaye amekabidhiwa wizara ya usalama wa ndani.

ECOWAS vile vile inalitaka bunge la Mali kujiuzulu na kuruhusu kuitishwa uchaguzi mpya.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW