1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Uchumi

Vita ya Iran yaiongezea Kenya Airways abiria

23 Machi 2026

Shirika la ndege la Kenya limesema abiria wanaotaka kusafiri kwa ndege hiyo wameongezeka kufuatia baadhi ya mashirika mengi ya eneo la Mashariki ya kati kusitisha safari zao

Shirika la ndege la Kenya Airways limekuwa likifanya safari zake katika maeneo mbali mbali ya dunia
Shirika la ndege la Kenya Airways limekuwa likifanya safari zake katika maeneo mbali mbali ya duniaPicha: picture-alliance/dpa

Shirika la ndege la Kenya, limesema mahitaji ya abiria ya kusafiri na ndege hiyo yameongezeka kufuatia athari zilizosababishwa na vita mashariki ya kati.

Ongezeko hilo la  abiria limeripotiwa zaidi katika kanda ya Ulaya Marekani na Asia.

Vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vimevuruga shughuli katika sekta ya usafiri wa anga na kusababisha baadhi ya mashirika ya ndege kuongeza bei pamoja na kubadilisha ratiba zao kupunguza vituo vya kusimama katika viwanja vya ndege vya eneo la Mashariki ya kati au wakati mwingine kufuta kabisa safari zao.

Mivutano inazidi kushuhudiwa katika Jumuiya ya EAC

Shirika la Kenya Airways limesema ongezeko la wateja wake limefikia asilimia 100 kutoka asilimia 70 mwezi Januari.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW