Kenya imemrejesha Sheikh Abdulla Al-Faisal nchini Jamaica
21 Januari 2010Matangazo
Abdulla Al- Faisal ambaye kuzuiliwa kwake kuliepelekea jamii ya waislam kufanya maandamano yaliyosababisha vifo vya watu wawili na wengine kadhaa kujeruhiwa wakiwemo maafisa wa usalama alitarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni baada ya wanaharakati wa haki za binadamu kuteta kwamba kuzuiliwa kwake ni kinyume cha sheria kwani alikuwa na stakabadhi za kuwa nchini Kenya.
Wakati huo huo, Msemaji wa serikali Dr. Alfred Mutua amekiri kwamba wanamgambo wa kundi la Al-Shabaab waliodaiwa kushiriki kwenye maandamano ya siku ya Ijumaa wametisha kuivamia Kenya.
Kutoka Nairobi Mwandishi wetu Alfred Kiti ametuandalia taarifa ifuatayo.