1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya kuendesha oparesheni kusaka majangili

Wakio Mbogo15 Machi 2023

Mamia ya watu wamelazimika kuyahama makazi yao kufuatia amri ya serikali iliyowapa saa 24 kuondoka maeneo 27 yanayoaminika kuwa maficho ya majangili, katika eneo hilo visa vya watu kuuwawa vimekuwa vikishuhudiwa.

Somalia Tabda|  Kenianische Soldaten | Militäroffensive
Picha: Ben Curtis/AP Photo/picture alliance

 Mashambulizi na mauaji katika maeneo hayo bado yanaendelea licha ya oparesheni ya kiusalama inayofanyika katika kaunti 6 zilizoainishwa kuwa hatari. 

Sammy Yatich aliamkia taarifa za mwanamme mmoja kuwawa na mifugo zaidi ya 200 kuibwa eneo anokoishi Baringo Kaskazini.

Majangili hao pia walitekeleza uvamizi mwingine mchana wa leo katika eneo la Baringo Kusini.

Soma pia:Serikali yawatafutia maji wafugaji Kenya

Mapema wiki hii Waziri wa usalama wa ndani Kithure Kindiki alitangaza masaa 24 kwa watu wanaoishi kwenye milima na mapango 27 katika kaunti 6 zilizoainishwa kama hatari kuyahama makaazi yao.

Hatua hii imechukuliwa na serikali ili kuwapa nafasi ya kukabiliana vilivyo na majangili wanaoaminika kutumia mapango na milima hiyo kama maficho yao.

"Atakayepatikana katika maeneo hayo kuanzia jumatatu  saa mbili wiki hii, atachukuliwa kuwa mshukiwa wa ujangili.” Alisema waziri wa usalama Kenya

Muda huo uliotolewa umekamilika, na taswira katika maeneo haya ni ya magari ya kijeshi yakikokota mizinga na zana za kivita za kukabiliana na magaidi, yakielekea maeneo ya oparesheni.

Shule zafungwa kupisha oparesheni

Shule nyingi katika maeneo haya zimeanza likizo fupi mapema ili waalimu na wanafunzi wasije wakapatikana hapa wakati wa oparesheni.

Wakaazi nchini Kenya wakiendelea na kazi zao za kila sikiPicha: Monicah Mwangi/Reuters

Lakini licha ya agizo hilo la serikali, wezi wa mifugo wameendelea kuwavamia na kuwaua watu wasiokuwa na hatia.

Wakaazi wanapinga amri ya serikali ya kuwahamishawakisema inayavuruga maisha yao.

Wengi hawajui pa kwenda na wanahofu iwapo wanakokwenda kuna usalama au watakutana na mauti yao.

Soma pia:Uamuzi wa Mahakama ya juu wawapa hofu viongozi wa dini Kenya

Akizungumza na kituo kimoja cha habari hii leo, Mbunge wa Kacheliba Titus Lotee ameikosoa serikali kwa kuiadhibu jamii nzima badala ya kuwaendea wahalifu.

"Kama Waziri anasema kwamba anataarifa kamili kuhusu watu wanaochochea uhalifu huu, kwa nini aadhibu jamii zote?"

Alihoji mwanasiasa huyo anaewakilisha eneo hilo katika bunge.

Oparesheni hii sasa inaongozwa na naibu mkuu wa polisi nchini Noor Gabow.

 

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW