1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya: Sharti wageni wathibitishe wamepata chanjo ya COVID

6 Desemba 2021

Serikali ya Kenya imetangaza sharti la raia wote wa kigeni wanaoingia nchini humo kuwa ni lazima wawe na cheti cha kuonyesha wamechomwa chanjo dhidi ya virusi vya korona kabla ya kuruhusiwa kuingia katika taifa hilo.

Kenia Streik der Kenya Aviation Workers Union
Picha: DW/S. Wasilwa

Kulingana na waziri wa afya Mutahi Kagwe, raia wote wa kigeni watatakiwa kuthibitisha kuwa wamepokea chanjo dhidi ya ugonjwa wa Covid 19 kwanza ndipo waruhusiwe kuingia nchini katika hatua hii inayolenga anga za usafiri za kuingia nchini Kenya.  

Waziri Kagwe amefafanua kuwa, hatua hii ni mojawapo ya mkakati wa serikali  katika kudhibiti makali ya kirusi cha korona cha Omicron. 

Itakumbukwa kuwa, serikali ya Kenya ilikuwa imeahidi, haitafunga mipaka yake licha ya kuibuka kwa kirusi cha Omicron.  

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW