1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya yatoa zabuni ya ujenzi wa uwanja mpya wa ndege

4 Machi 2026

Kenya imetoa zabuni ya ujenzi wa uwanja mpya wa ndege karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa (JKIA) mjini Nairobi. Haya ni kwa mujibu wa waziri wa uchukuzi nchini humo, Davis Chirchir.

Uwanja wa ndege wa JKIA
Abiria wakiwa nje ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) mjini Nairobi nchini Kenya mnamo Novemba 7, 2022Picha: Billy Mutai/AA/picture alliance

Katika taarifa jana jioni, Chirchir alisema kuwa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini humo, ilitoa zabuni ya kujenga uwanja mpya wa ndege karibu na JKIA, na kuboresha maeneo ya uwanja uliopo.

Zabuni hiyo ni kwa ajili ya ujenzi wa kituo kipya cha kushughulikia abiria milioni 10 kila mwaka pamoja na kutengeneza njia mpya za kuruka kwa ndege miongoni mwa mambo mengine.

Mnamo mwezi Novemba 2024, Rais wa Kenya William Ruto aliagiza kufutiliwa mbali kwa mchakato wa ununuzi ambao ungewezesha kampuni moja ya India kwa jina Adani Group kudhibiti uwanja huo wa ndege wa JKIA kufuatia kufunguliwa mashitaka kwa mwanzilishi wake, Gautam Adani, nchini Marekani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW