Kenya yasherehekea Eid ul Fitr kwa kuombea amani
20 Machi 2026
Mbali ya kutakiana neema na baraka za sikukuu hii, waumini walipongezana kwa kukamilisha mfungo wa Ramadhan na kuhimizana kuwakumbuka wengine katika jamii kipindi hiki cha sherehe hasa walio katika mazingira magumu baadhi wakielezea utofauti wa mitindo ya jinsi hali zilivyobailika katika kukirimiana.
Suleiman Mohamed ni miongoni mwa waumini hao amesema "Kuhimiza, binadamu warudi kwa ule usawa wa zamani, kuwa na utu, jirani hata kama sio Muislamu una upendo naye sana yani lakini dunia ya sahii sijui tunaelekea wapi, ukiangalia sahii huko Gaza, tusiende mbali hapa tu Sudan baina ya Wao kwa wao wanapigana."
Kilele cha Swala ya Eidni hotuba kwa waumini, mashekhe kutoka maeneo mbali mbali ikiwemo Kisumu na Nairobi wakitumia majukwaa yao kukumbuka wahanga wa vita vinavyoendelea katika sehemu mbali mbali za ulimwengu.
Umma waomba kuendeleza matendo mema
Kadhalika, wamehimiza umma kuendelea na utekelezaji wa amali njema ikiwemo kuendekeza ibada ya swala, kusoma Quran na kufanya kheir, msisitizo wa, waishi walivyokuwa kwenye Ramadhani.
Sheikh Adan Kala wa msikiti wa Jamia Kisumu na Sheikh Jamaludeen Osman wa msikiti wa Jamia Nairobi amesema "Hakuna neema kubwa kama neema ya Amani, hakuna neema kubwa kama neema ya Afya, ya rizki na watoto na mali hakuna neema kubwa kama Mwenyezi MUNGU kukuepusha na balaa za duniani leo ni siku ya furaha, leo ni siku ya kheir, bila kuwasahau ndugu zetu waliokosa neema ya amani tuwakumbuke kwa dua."
Ibada ya funga kwa waumini wa dini hii, inakamilika huku wenzao waumini wa dini ya Kikristo wakiendelea na mfungo wa Kwaresma itakayokamilika kwa maadhimisho ya Pasaka, mfungo unaojumuisha jumla ya siku 40 huku mfungo wa Kiislamu ukijumuisha mfululizo wa siku 30.