1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Afrika Mashariki iendelee kuleta amani Kongo - Kenyatta

13 Julai 2023

Rais wa zamani wa Kenya, Uhuru Kenyatta, ametoa wito wa kusuluhisha kwa njia ya amani mzozo wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, akisema harakati tofauti za kikanda zinapaswa kuendelea.

Kenia Nairobi | Jubilee Party hält National Delegates Council trotz interner Krise ab
Picha: Shisia Wasilwa/DW

Kenyatta, ambaye ni msuluhishi katika mzozo huo, aliyasema hayo katika mkutano uliofanyika mjini Goma ambao uliwakutanisha viongozi wa serikali ya Kongo, wawakilishi wa Umoja wa Mataifa pamoja na wanadiplomasia wa Magharibi.

Soma zaidi: Kagame amtuhumu Tshisekedi kutumia mzozo wa M23 kujinufaisha kisiasa

Rais huyo wa zamani wa Kenya amesisitiza kuwa watu milioni mbili waliolazimika kukimbia mzozo huo wanapaswa kuruhusiwa kurejea salama na lazima uhuru wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo uheshimiwe.

Soma zaidi: Kenyatta atoa wito wa kupunguza mzozo DR Kongo

Kundi la waasi wa M23, ambalo lilichukua udhibiti wa maeneo kadhaa, linataka mazungumzo na serikali ya Kinshasa ambayo imetupilia mbali azma hiyo.

Badala yake serikali ya Kongo inalitaka kundi hilo kujisalimisha bila masharti na kuondolewa kwa wanajeshi wa Rwanda wanaodai wanawasaidia waasi wa M23.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW