1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KHARTOUM: Rais Bashir alipongeza kundi la SPLM

11 Agosti 2005

Rais Omar el- Bashir wa Sudan amelipongeza kundi la SPLM nchini humo kwa kuonyesha ushujaa baada ya kifo cha John Garang. Katika sherehe ya kuapishwa Silva Kiir, kuwa makamu wa rais wa Sudan, rais Bashir amesema leo ni siku ya huzuni na furaha kwa Sudan.

Kiir ameichukua nafasi iliyowachwa na marehemu John Garang, aliyefariki dunia katika ajali ya helikopta majuma mawili yaliyopita. Ameapa kuuendeleza mpango wa amani uliosainiwa mwezi Januari mwaka huu unaolenga kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya eneo la kazkazini na kusini, ambavyo vilisababisha vifo vya watu milioni mbili. Kiir ameahidi pia kufuata nyayo za Garang na kuimarisha umoja wa taifa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW