Kikao cha kilele chaanza Copenhagen
7 Desemba 2009Matangazo
Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na athari za mabadiliko ya hali ya hewa Yvo de Boer amewatolea wito viongozi wa ulimwengu kuwa na msimamo wa pamoja wakati ambapo kikao cha kilele cha mazingira kinaanza rasmi hii leo.
De Boer alisema kuwa kuna haja ya kila nchi kutangaza bayana mchango wao ili mkutano huo uweze kufanikiwa.
Lengo la kikao hicho cha siku kumi na mbili ni kufikia mkataba mpya utakaosaidia kuvipunguza viwango vya gesi za viwanda baada ya ule uliopo wa Kyoto kumaliza muda wake ifikapo mwaka 2012.