1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kikosi cha kulinda amani Haiti chaahidi kuleta utulivu

9 Julai 2024

Mkuu wa kikosi cha jeshi la polisi la Kenya, linaloongoza kikosi cha kimataifa cha kupambana na magenge ya uhalifu nchini Haiti,amesema hakuna nafasi ya kushindwa katika juhudi hizo za kuleta utulivu nchini humo.

KEnya | Kikosi cha Kenya ambacho kilinda amani Haiti
Rais Ruto akiwaaga askari wa Kenya ambao ni miongoni mwa Ujumbe wa Kimataifa wa kulinda amani Haiti.Picha: REBECCA NDUKU/PRESIDENTIAL COMMUNICATION SERVICE/EPA

Kamanda huyo wa kikosi cha askari wa Kenya,Godfrey Otunge amesema  Ujumbe huo unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa uko tayari kuhakikisha chaguzi za kidemokrasia zinafanyika katika taifa hilo la Carribean.
 
"Tunakazi tuliyojitolea kuifanya.Na kwahivyo tunapswa kuifanya kwa viwango vya ubora kadri ya uwezo wetu na kuleta mafanikio. Kazi yetu ni kuhakikisha tunarudisha amani kote nchini Haiti.''

Soma pia:Polisi wa Kenya waendelea kuwasili Haiti kuyadhibiti magenge

Ni mara ya kwanza kwa jeshi la polisi la Kenya lililoko Haiti kutowa tamko kwa umma,kupitia mkutano na waandishi habari uliooneshwa kwenye kituo cha habari cha taifa, nchini Haiti.

Kikosi cha askari wa Kenya kinatarajia kuungana baadae na askari kutoka Bahamas,Bangladesh,Barbados,Benin,Chad na Jamaica katika harakati za kuyakabili magenge ya Haiti.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW