1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kikosi cha MONUSCO chaondoka rasmi Kivu Kusini

25 Juni 2024

Kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa, MONUSCO hatimae kimefunga virago vyake na kuondoka Kivu kusini katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

DR Kongo MONUSCO
Kikosi cha MONUSCO chaondoka rasmi Kivu KusiniPicha: AA/picture alliance

Hafla yakuondoka imefanyika katika Kijiji cha Kavumu kwenye umbali wa kilomita 33 kaskazini mwa mji wa Bukavu ambako ameshiriki pia waziri Mkuu wa Congo Judith Suminwa Tuluka. 

Katika hafla hiyo Mkuu wa  Tume ya Amani ya Umoja wa Mataifa Nchini Congo Monusco Bintou Keita ameishukuru serikali ya Kongo kwa ushirika wake katika kufanikisha amani lakini pia kusisitiza kwa mara nyingine kwamba baada ua Monusco kuondoka, Serikali ya Congo inabaki na wajibu mkubwa kulinda raia wake.

Kivu Kusini inakabiliwa na kitisho baada ya jeshi la Umoja wa Mataifa kuondoka

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani , Naibu Waziri Mkuu anayeshughulikia Mambo ya Ndani Jacquemin Shabani alikiri kuwa hali ya usalama bado ni tete na kuahidi kuwa juhudi zitafanyika kuhakikisha usalama katika jimbo zima la Kivu Kusini. Jacquemin Shabani anaeleza.

MUNUSCO imekuwa katika operesheni ya moja kwa moja ya ardhini nchini Kongo tangu mwaka 2002, ikiwa na wajibu mkubwa wa kulisadia jeshi la taifa hilo katika wajibu wa kuwalinda watu wake. Baada ya Kivu Kusini, MONUSCO inakusudia kuendelea na mchakato wa kujiondoa katika majimbo ya Kivu Kaskazini, na Ituri. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW