1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kikosi cha RSF chadai jeshi la Sudan limeshambulia Khartoum

15 Mei 2023

Kikosi cha msaada wa dharura nchini Sudan, RSF, kimelishutumu jeshi la Sudan kwa kuishambulia hospitali moja kwa ndege za kivita katikati mwa mji mkuu, Khartoum.

Sudan Khartum | Kämpfe zwischen Armee und RSF-Miliz | General Mohamed Hamdan Dagalo
Picha: MOHAMED NURELDIN ABDALLAH/REUTERS

Taarifa iliyotolewa na kikosi hicho cha RSF imesema leo kwamba mashambulizi hayo "yaliua na kuwajeruhi mamia ya watu wasiokuwa na hatia."

Hata hivyo, madai hayo ya mashambulizi bado hayajathibitishwa na taasisi ya kujitegemea, ingawa baadhi ya mashuhuda wameandika kwenye mtandao wa Twitter kuwa mashambulizi hayo yalitokea mapema mwezi huu.

Mashambulizi yaendelea Khartoum wakati wapinzani wakikutana Saudia

Shirika la misaada la CARE limetahadharisha kuwa mzozo huo unaweza kulemaza sekta ya afya hasa katika mji mkuu, Khartoum, ambako karibu theluthi mbili ya vituo vya afya bado vimefungwa - kimoja tu kati ya vituo sita vya afya ndicho kinachofanya kazi kwa sasa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW