Kilimo barani afrika bado kinahudumu katika mwendo taratibu kutokana na uhaba wa teknolojia na nyenzo mbali mbali za kufanya kilimo chenye tija. George Waloma kijana kutoka Tanzania amethubutu kufanya kilimo chenye kutumia mbolea ambayo inatokana na kinyesi cha kuku na kurudufishwa kupitia mfumo wa kumwagilia kwa matone kwa ajili ya kukuza bustani za mboga mboga.