1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Kim Jong Un akutana na waziri wa ulinzi wa Urusi

27 Julai 2023

Kim Jong Un amekutana na waziri wa Ulinzi wa Urusi Sergei Shoigu kujadili masuala ya kijeshi na mazingira ya usalama wa kikanda.

Nordkorea | Sergei Schoigu und Kim Jong Un
Picha: KCNA/REUTERS

Mjumbe huyo wa Rais Vladimir Putin amekutana na kiongozi wa Korea Kaskazini wakati ambapo nchi hiyo iliyojitenga na mataifa mengine ulimwenguni ikiadhimisha miaka 70 tangu vita vya Korea vya kati ya mwaka 1950-1953 vilipositishwa.

Katika mkutano huo, Shoigu anaripotiwa kumuwasilishia Kim barua "nzuri" iliyotiwa saini na Rais Vladimir Putin.

Soma zaidi: Kim Jong Un akutana na ujumbe wa China

Hata hivyo, haikuwekwa wazi masuala ya kijeshi yaliyojadiliwa katika mkutano wa viongozi hao wawili.

Korea Kaskazini imekuwa ikiiunga mkono Urusi katika vita vyake na Ukraine ikisema nchi za Magharibi zinazoongozwa na Marekani, ndizo zilizoipelekea Urusi kuchukua hatua za kulinda maslahi yake ya kiusalama. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW