Kimbunga NOEL kinaelekea Kanada
3 Novemba 2007Matangazo
Rais Felipe Calderon wa Mexico amesema,vikosi vyote vya anga vinasaidia kupeleka misaada kwa watu waliozingirwa na mafuriko.Asilimia 80 ya jimbo la Tabasco limefurika.
Hata visiwani Jamaika,Kuba na Bahamas kimbunga NOEL kimesababisha mafuriko na hasara kubwa.Maelfu ya watu hawana pa kuishi na wanangojea misaada.Hadi watu 120 wamepoteza maisha yao katika eneo la Karibik na wengi wengine hawajulikani walipo.Sasa kimbunga hicho kinaelekea upande wa Kanada.