1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaAsia

Kimbunga Yagi chasababisha vifo vya watu 4 Vietnam

7 Septemba 2024

Mamlaka nchini Vietnam zimesema dhoruba iliyotokana na kimbunga Yagi imewaua watu wasiopungua 4 na kuwajeruhi wengine 78 kaskazini mwa taifa hilo.

Asia -  Kimbunga Yagi
Kimbunga Yagi kikiwasili Vietnam na upepo wa kasi kubwa. Picha: NHAC NGUYEN/AFP

Kimbunga ambacho kimetajwa na mamlaka za Vietnam kuwa ndiyo kikubwa zaidi kuipiga nchi hiyo katika kipindi cha miongo kadhaa iliyopita, kiliwasili kaskazini mwa nchi hiyo mchana wa leo baada ya kufanya uharibifu nchini China na Ufilipino.

Kimeipiga miji miwili ya Quang Ninh na Haiphong kikisafiri kwa kasi ya kilometa 149 kwa saa. Safari kadhaa za majini zimesitishwa kwenye mji wa Quang Ninh wenye shughuli nyingi za utalii za kukitembelea kisiwa cha Ha Long Bay ambayo ni moja ya turathi ya ulimwengu.

Hapo jana kimbunga Yagi kilifanya uharibifu mkubwa wa miundombinu ya nishati na barabara kwenye kisiwa cha China cha Hainan,na mamlaka zimesema watu wawili walikufa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW