1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaAsia

Kimbunga Yagi chawasili Vietnam baada ya kuipiga China

7 Septemba 2024

Kimbunga Yagi ambacho ndiyo kikubwa zaidi kurikodiwa kwa mwaka huu barani Asia, kimewasili kaskazini mwa Vietnam leo baada ya kulipiga eneo la kusini mwa China jana na kusababisha maafa ikiwamo vifo vya watu wawili.

Asia -  Kimbunga Yagi
Athari za kimbunga Yagi kwenye kisiwa cha Hainan, China. Picha: CNS/AFP

Kimbunga hicho kilianzia nchini Ufilipino mapema wiki hii na kusababisha vifo vya watu 16 na hapo jana kiliwasili kwenye kisiwa cha China cha Hainan, na dhoruba yake iling´oa miti na kuharibu miundombinu ya nishati na barabara.

Mamlaka za Vietnam zimesema kilipowasili mapema leo asubuhi kwenye mji wa pwani wa Haiphong kilikuwa kinasafiri kwa kasi ya kilometa 160 kwa saa.

Sehemu ya mji huo ulio na idadi kubwa ya viwanda imeshuhudia uharibifu kidogo kwenye majengo na huduma ya umeme pia imetatizika.

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW