1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KINSHASA

16 Februari 2005

Wanafunzi tisa wa shule wameuawa kwa kupondwa na mawe baada ya lori lililokuwa limejaza mawe kuwaangukia katika mji wa kusini wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Wanafunzi hao walikuwa ndio kwanza wanatoka shuleni na walikuwa wanasubiri kuvuka barabara ndipo walipoangukiwa na mawe yaliyokuwa yamejazwa katika lori moja,baada ya dereva wake kushindwa kulimudu.

Ajali hiyo imetokea kilometa 20 kutoka mji wa Lubumbashi mji mkuu wa jimbo la kusini-mashariki la Katanga.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW