KINSHASA:Mwanamuziki maarufu barani afrika afariki ghafla
11 Agosti 2007Matangazo
Mwanamuziki mashuhuri barani afrika, Madilu System amefariki dunia ghafla leo hii mjini Kinshasa katika Jamuhuri ya Kidemokrasi ya watu wa Kongo.
Madilu System amefariki kutokana na shinikizo la moyo baada ya kufikishwa katika hospitali mmoja leo asubuhi mjini Kinshasa.
Mwanamuziki huyo ambaye alijipatia umaarufu mkubwa barani afrika, alikuwa akijianda kutumbuiza katika tamasha kubwa leo hii jijini Kinshasa.