1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Haniyeh afanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Uturuki

21 Januari 2024

Kiongozi wa kundi la Hamas anayeishi nchini Qatar Ismail Haniyeh, amekutana kwa mazungumzo na Waziri Mkuu wa Uturuki Hakan Fidan ikiwa ni mkutano wao wa kwanza ndani ya zaidi miezi mitatu.

Qatar Doha | Kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh.
Kiongozi wa kundi la Hamas Ismail Haniyeh.Picha: Iranian Foreign Ministry/ZUMA Wire/IMAGO

Wanamgambo wa Hamas waliwachukua mateka zaidi ya watu 250 wakati walipoishambulia Israel Oktoba 7 na kuachiwa kwa mateka waliobakia pamoja na kusimamishwa kwa mapigano haraka iwezekanavyo, ndio mambo waliyoyajadili viongozi hao wawili walipokutana Uturuki. 

Kulingana na duru za mkutano, Haniyeh na Fidan pia walijadili kuhusu kuongeza msaada wa kiutu mjini Gaza na pia suluhisho la kuwa na mataifa mawili kwaajili ya amani ya kudumu ya Israel na Palestina. 

Kiongozi wa Hamas asema wako tayari kwa utawala mmoja wa Wapalestina

Israel imeapa kulisambaratisha kundi la Hamas kufuatia hatua yake ya kulishambulia Oktoba 7 na kusababisha mauaji ya waisraeli 1,140. Mashambulizi yanayoendelezwa na Israel katika ukanda wa Gaza hadi sasa yamesababisha mauaji ya wapalestina zaidi ya 24,000.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW