1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBurkina Faso

Traore: Uchaguzi "sio kipaumbele" Burkina Faso

30 Septemba 2023

Kiongozi wa kijeshi nchini Burkina Faso Kapteni Ibrahim Traore amesema uchaguzi nchini humo sio "kipaumbele" ikilinganishwa na hali ya "usalama."

Kiongozi wa kijeshi wa Burkina Faso Ibrahim Traore
Kiongozi wa kijeshi wa Burkina Faso Ibrahim TraorePicha: Vladimir Smirnov/TASS/IMAGO

Traore ameeleza kuwa, hakutafanyika uchaguzi hadi nchi hiyo itakapokuwa salama na kumuwezesha kila mtu kupiga kura.

Traore ameyasema hayo katika hotuba iliyopeperushwa moja kwa moja kwenye televisheni ya taifa, karibu mwaka mmoja baada ya kuingia madarakani kwa njia ya mapinduzi.

Kiongozi huyo wa kijeshi, ambaye ameahidi kuirejesha Burkina Faso kwa utawala wa kidemokrasia na kufanya uchaguzi mnamo Julai mwaka 2024, pia ametangaza mabadiliko ya katiba ili kuwakilisha sura ya kitaifa.

Wakati Traore alipotwaa madaraka, alijipa "miezi miwili hadi mitatu" kuimarisha usalama, ila mwaka mmoja baadae nchi hiyo ya Afrika Magharibi bado inakabiliwa na mashambulizi kutoka makundi ya wanamgambo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW