1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMadagascar

Kiongozi wa kijeshi Madagascar kuapishwa rasmi kuwa rais

15 Oktoba 2025

Kiongozi mpya wa kijeshi wa Madagascar Kanali Michael Randrianirina ataapishwa rasmi kuwa rais wa nchi hiyo katika siku zijazo.

Madagascar | Kanali Michael Randrianirina akitangaza kuwa jeshi limetwaa madaraka
Kiongozi mpya wa kijeshi wa Madagascar Kanali Michael Randrianirina akitoa taarifa kwa umma kwamba jeshi limetwaa madaraka.Picha: Brian Inganga/AP Photo/picture alliance

Hayo yameelezwa na vyanzo viwili vya kuaminika baada ya kufanyika mapinduzi ya kumuondoa madarakani rais  Andry Rajoelina  aliyeikimbia nchi baada ya wiki kadhaa za maandamano ya umma kufuatia uhaba wa maji na kukatika kwa umeme.

Marekani imewatolea wito wadau wote nchini Madagascar kutafuta suluhisho la amani linaloheshimu katiba baada ya kikosi maalumu cha jeshi CAPSAT kutwaa madaraka.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW