SiasaNamibia
Kiongozi wa Namibia aliyepigania uhuru Sam Nujoma azikwa
1 Machi 2025
Matangazo
Nujoma, aliyeongoza kundi la wapiganaji wa SWAPO kutetea uhuru wa taifa hilo la kusini mwa Afrika, alifariki Februari 9 mwaka huu akiwa na umri wa miaka 95. Rais wa sasa wa Namibia Nangolo Mbumba aliongoza mkusanyo huo na kumtaja Nujoma kama kiongozi mashuhuri ambaye urathi wake utakuwa nguzo ya kudumisha umoja.
Soma pia: Viongozi mbalimbali waomboleza kifo cha Sam Nujoma
Viongozi kadhaa wa Afrika akiwemo Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, Joao Lourenco wa Angola, Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe na maafisa wa kigeni kama spika wa bunge la Cuba Esteban Lazo Hernandez wamehudhuria maziko yaliyofanyika muda mfupi baadaye na kupeperushwa moja kwa moja kupitia televisheni ya taifa.