1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Kiongozi wa upinzani wa Taiwan aitembelea China

7 Aprili 2026

Ziara ya Cheng Li wun inafanyika katikati ya kiwingu cha kuongezeka mivutano kati ya Beijing na Taipei.

Kiongozi wa KMT Cheng Li-wun akiwa amewasili Shanghai
Kiongozi wa KMT Cheng Li-wun akiwa amewasili Shanghai Picha: Lu Chia-jung/Central News Agency/AFP

Kiongozi wa upinzani wa Taiwan Cheng Li wun ameanza ziara ya kuitembelea China, kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 10. Kiongozi huyo wa chama cha Nationalist aliwasili leo Jumanne katika mji wa Shanghai akiandamana na ujumbe wake.

Ziara hiyo inafanyika katikati ya kiwingu cha kuongezeka mivutano kati ya Beijing na Taipei. Ziara ya mwisho kuwahi kufanywa na kiongozi wa chama hicho cha upinzani kinachoegemea upande wa Beijing, kinachofahamika pia kama Kuomintang au KMT ni mwaka 2016 wakati kikiongozwa na Hung Hsiu-chu.

China yaendelea na luteka yake ya kijeshi karibu na Taiwan

Kiongozi wa sasa,Cheng Li wun amesema anataraji ziara yake itatowa mwanga kwa jamii ya Kimataifa kuona fursa ya kutatua mivutano kwa njia za kidiplomasia na kuepusha vita.

Hata hivyo serikali ya Taiwan imemtahadharisha kiongozi huyo wa upinzani dhidi ya kujichukulia maamuzi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW

Taarifa zaidi kutoka DW