Kiongozi wa zamani wa Indonesia Suharto amefariki hospitali
27 Januari 2008Matangazo
JAKARTA:
Kiongozi wa zamani wa Indonesia,Suharto amefariki dunia akiwa na miaka
86.Kiongozi huyo alikuwa akiugua tangu muda mrefu na alipelekwa tena hospitali katika mji mkuu Jakarta wiki tatu za zilizopita.Suharto alitawala nchini Indonesia kuanzia mwaka 1967 hadi 1998.Hadi wanasiasa elfu moja wa upande wa upinzani waliuawa wakati wa utawala wake mrefu wa mabavu.
Aliondoka madarakani kufuatia maandamano makubwa ya upinzani kuhusika na ulajirushwa na ukiukaji wa haki za binadamu.Licha ya kukabiliwa na mashtaka ya ubadhilifu wa mali ya serikali na ukiukaji wa haki za binadamu,mawakili wake walifaulu kumzuia kufikishwa mahakamani kwa sababu ya hali mbaya ya afya.