1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa zamani wa Myanmar Win Myint aachiliwa huru

17 Aprili 2026

Rais wa zamani Myanmar Win Myint aliyekuwa akishikiliwa kizuizini tangu baada ya mapinduzi ya kijeshi yaliyofanyika mwaka 2021 ameachiliwa huru kwa msamaha wa Rais Min Aung Hlaing.

Naypyidaw | Aung San Suu Kyi na Win Myint mahakamani
Rais wa zamani wa Myanmar Win Myint na aliyekuwa kiongozi wa kiraia Aung San Suu Kyi walipokuwa mahakamani Mei 24.2021Picha: Myanmar Ministry of Information/AFP

Taarifa iliyotolewa na televisheni ya taifa ya nchi hiyo imesema hatua hiyo ni sehemu ya msamaha uliotolewa na kiongozi wa Myanmar Aung Hlaing kwa jumla ya wafungwa 4,335. Myint alihukumiwa kifungo cha miaka 12 jela kwa makosa mbalimbali yakiwemo uchochezi, udanganyifu wa uchaguzi na rushwa.

San Suu Kyi apunguziwa adhabu ya kifungo

Aidha kiongozi wa zamani Aung San Suu Kyi amepunguziwa pia kifungo cha miaka 27 anachoendelea kukitumikia. Suu Kyi alihukumiwa kwa makosa mbalimbali yakiwemo rushwa na uchochezi. Katika hatua nyingine  Rais Min Aung Hlaing amebadilisha hukumu zote za kifo kuwa vifungo vingine katika msamaha alioutoa Ijumaa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW