1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Klabu ya Arsenal yafuzu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya

6 Mei 2026

Klabu ya Arsenal imefuzu kwa fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya baada ya kupata ushindi wa 1-0 dhidi ya Atletico Madrid katika uwanja wa Emirates na hivyo kushinda kwa jumla ya mabao 2-1.

Ligi ya mabingwa 2025/26 | Nusu Fainali | Arsenal vs. Atlético Madrid
Wachezaji wa Arsenal washerehekea ushindi wao dhidi ya Atlético Madrid baada ya kufuzu kwa fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya katika uwanja wa Emirates Mei 5, 2026Picha: Dylan Martinez/REUTERS

Bao hilo la pekee lilifungwa na nahodha Bukayo Saka muda mfupi kabla ya kipindi cha kwanza kukamilika.

Hii ni mara ya kwanza katika muda wa miaka 20 kwa Arsenalkufika fainali ya michuano hiyo, mara ya mwisho ikiwa mwaka 2006 ambapo ilipoteza dhidi ya Barcelona.

Vijana wa Mikel Arteta sasa wanasubiri mshindi kati ya Bayern Munich na Paris Saint-Germain katika fainali itakayochezwa mjini Budapest Mei 30.

Ushindi huo pia unaiweka Arsenal katika nafasi nzuri ya kushinda mataji mawili msimu huu: Ligi Kuu ya Uingereza na Ligi ya Mabingwa barani Ulaya.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW