1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kombe la Dunia: Matumaini ya Rwanda yafifia

Saumu Njama Christopher Karenzi
13 Oktoba 2025

Timu ya taifa ya Rwanda Amavubi, matumaini ya kufuzu kombe la dunia la mwaka 2026, tayari yamefifia baada ya kufungwa na Benin 1-0 jijini Kigali.

Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Rwanda
Wachezaji wa timu ya Taifa ya Rwanda washerekea ushindi baada ya kuilaza Afrika Kusini kwenye mashindano ya kuwania kufuzu kwa Kombel la Dunia 2026.Picha: Julius Ntare/empics/picture alliance

Kocha wa timu ya taifa ya Rwanda, Adel Amrouche, amefichua kuwa aliumizwa sana na kushindwa kwa timu yake mbele ya mashabiki wa nyumbani akiwepo pia Rais wa Rwanda Paul Kagame. Amewataka  mashabiki kutokata tamaa.

"Tumeumia sana, lakini huu siyo mwisho wa maisha, huu ni mpira wa miguu. Tunaweza kuiona Rwanda kwenye AFCON  niamini."

Aidha Kocha Amrouche amewaasa wanyarwanda kuendelea kuipenda timu yao ya  taifa na kupuuza tetesi zisizo na msingi, akisisitiza kuwa Amavubi (Timu ya taifa ya Rwanda) itaendelea kujengwa, iwe ni yeye au kocha au mwingine.

Kesho  jumanne itacheza mechi yake ya mwisho ya kufuzu kwa Kombe la Dunia 2026, ambapo imesafiri kuikabili Afrika Kusini.mjini Nelpsuuits.

Ushindi huo haukumaliza tu kampeni ya Rwanda bali pia umebadilisha mwelekeo wa kilele cha Kundi C. Benin sasa imekaa kileleni ikiwa na pointi 17, ikizidi Nigeria kwa pointi tatu kuelekea michezo ya mwisho ya makundi.

Muelekeo wa kundi C

Mechi za kufuzu Kombe la Dunia 2026, Rwanda ikichuana na Afrika Kusini katika uwanja wa Huye Stadium in Butare, Rwanda.Picha: Julius Ntare/Sports Inc/empics/picture alliance

Matokeo hayo pia ni pigo kubwa kwa matumaini ya Nigeria ya kufuzu. Licha ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Lesotho, Super Eagles sasa hawana udhibiti kamili wa hatima yao.

Katika mchezo mwingine muhimu wa kundi hilo, Zimbabwe na Afrika Kusini zilitoka sare baada ya pambano gumu, jambo lililozidi kufanya ushindani wa kufuzu kuwa mkali zaidi.

Kocha mkuu wa Benin Gernot Rohr, akiongea na vyombo vya habari amesema kwamba atakuwa na kibarua kesho na Super Eagles.

"Ingekuwa vyema zaidi kama Zimbabwe ingefunga bao, mambo yangekuwa mazuri, kwa sababu timu tatu zote zina nafasi ya kufuzu.

Tuna mechi ngumu zaidi. Ninawajua vizuri sana, si rahisi kushinda, hasa kwa kuwa Super Eagles wana nafasi ya kufuzu.

Kwa hiyo hii ni fainali  leo ilikuwa kama nusu fainali, sasa tunakwenda kucheza fainali."

Kwa sasa, Rwanda inashika nafasi ya nne kwenye kundi C ikiwa na alama 11, huku Benin ikiongoza kwa alama 17, Afrika Kusini ikiwa ya pili kwa alama 15, na Nigeria ikiwa ya tatu kwa alama 14.