1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kongamano la Vyombo vya Habari (GMF) laanza mjini Bonn

7 Julai 2025

Kongamano la Kimataifa la siku mbili la vyombo vya habari lililoandaliwa na Deutsche Welle (GMF) limefunguliwa katika mji wa Bonn, ulio magharibi mwa Ujerumani.

Global Media Forum 2025 | Bonn
Kongamano la Kimataifa la Vyombo vya Habari linaloandaliwa na Deutsche Welle (GMF) laanza mjini BonnPicha: Björn Kietzmann/DW

Wawakilishi wa vyombo vya habari kutoka pande zote za dunia watajadiliana kuhusu mikakati ya kuleta mshikamano katika kipindi hiki kilichogubikwa na migawanyiko duniani na katika wakati ambapo dunia inakabiliwa na tawala za kimabavu na kubinywa kwa uhuru wa habari.

GMF: Kuchangiana Masuluhisho dunia inapokabiliwa na migogo

Shirika la habari la kimataifa la DW linakusudia kukabiliana na hali hiyo kupitia jukwaa hili la habari la siku mbili linaloanza hii leo na kumalizika hapo kesho Jumanne

Kauli mbiu ya Kongamano la mwaka huu ni "Kuvunja vizuizi na kujenga madaraja."
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW