1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaJamhuri ya Kongo

Kongo-Brazzaville yapiga kura katika uchaguzi wa rais

Saleh Mwanamilongo
15 Machi 2026

Wananchi wa Jamhuri ya Kongo-Brazzaville wanapiga kura leo Jumapili kumchagua rais mpya, huku rais wa sasa, Denis Sassou Nguesso, akigombea muhula wa tano mfululizo.

Jamhuri ya Kongo Brazzaville 2021 | Wafuasi wanasherehekea kuchaguliwa tena kwa Rais Denis Sassou Nguesso
Kura ya maoni ya kikatiba mwaka 2015 iliondoa kikomo cha umri na mihula ya urais, na kumruhusu Sassou Nguesso kugombea tena na tenaPicha: Olivia Acland/REUTERS

Takribani wapiga kura milioni tatu wamejiandikisha kushiriki katika uchaguzi huo.

Hata hivyo, hali ya uchaguzi inaonekana tulivu hasa miongoni mwa vijana wengi ambao wanaamini kuwa rais huyo wa muda mrefu ataendelea kushinda. Vyama kadhaa vya upinzani pia vimetangaza kususia uchaguzi huo vikidai kuwa hauko huru na wa haki.

Kwa mujibu wa wachambuzi, wagombea sita wanaoshindana na Denis Sassou Nguesso hawana uwezo mkubwa wa kumzuia kuendelea kubaki madarakani. Rais huyo amekuwa madarakani kwa jumla ya miaka 42.

Uchaguzi huu unafanyika wakati nchi hiyo yenye utajiri wa mafuta inakabiliwa na madeni makubwa ya kimataifa na ukosefu mkubwa wa ajira kwa vijana. Zaidi ya nusu ya wananchi wa Jamhuri ya Kongo wanaishi katika umaskini.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW