Kongo kupiga maarufuku magari yenye usukani upande wa kulia
5 Julai 2007
Waziri wa uchukuzi na mawasiliano katika jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo amepiga maarufuku uendeshaji wa magari yanayotumia usukani upande wa kulia akidai sheria ya nchi hiyo hairuhusu magari hayo.
Matangazo
Aidha amesema ajali nyingi husababishwa na magari hayo. Hata hivyo hatua hiyo imewakasirisha raia wengi kama anavyoarifu mwandishi wetu John Kanyunyu kutoka Beni.