1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kongo na Rwanda kuja na rasimu ya makubaliano ya amani

26 Aprili 2025

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda zimeapa kuja na rasimu ya makubaliano ya amani ifikapo Mei 2 mwaka huu na kujizuia kuyasaidia kijeshi makundi ya wanamgambo.

DR Kongo Bukavu 2025 | M23
Wanamgambo wa M23 wakiwa wamesimama mbele ya umati wa watu huko Bukavu, Kivu Kusini Februari 28, 2025Picha: Ernest Muhero/DW

Haya ni kulingana na makubaliano yaliyotiwa saini na mataifa hayo mawili jana mjini Washington, Marekani, kama sehemu ya juhudi za kidiplomasia za kumaliza ghasia huko mashariki mwa Kongo.

Hatua hiyo inaibua matumaini kwamba mapigano yaliyoshuhudiwa hivi karibuni katika mzozo uliodumu kwa miongo kadhaa huenda yakapungua, licha ya miito ya kusitisha mapigano kutozaa matunda.

Pande zote mbili aidha zimekubaliana kushirikiana katika uratibu wa kukabiliana na makundi yenye silaha na mitandao ya uhalifu.

Makubaliano hayo yaliyofikiwa katikati ya hatua kubwa zilizopigwa na waasi wa M23, yanatarajiwa pia kufungua milango ya uwekezaji mkubwa wa Marekani kwenye ukanda huo wenye hifadhi kubwa ya madini ikiwa ni pamoja na dhahabu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW