1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Korea Kaskazini bado inataka mwafaka na Marekani

1 Machi 2019

Vyombo  vya habari  vya  taifa  nchini  Korea  Kaskazini  vimepuuzia  kutopatikana  makubaliano  katika  mkutano  wa  kilele kati ya  kiongozi wa  nchi  hiyo Kim Jong Un  na  rais Donald Trump wa Marekani.

USA-Nordkorea Gipfel - Donald Trump, Kim Jong Un
Picha: picture-alliance

Kauli kali ambazo  zilifuatia  mazungumzo  ya  mwanzo  yaliyoshindwa  kuhusiana  na  mpango wa silaha  za  kinyuklia  wa  Korea  kaskazini  na  vikwazo,  hazikuwapo  kwa  kiasi  kikubwa  mara hii, lakini  kulikuwa  na  hali  ya  kuutangaza  mkutano  huo  wa  siku  mbili   katika   mji  mkuu  wa Vietnam, Hanoi kwa  kiasi  fulani  kwa  hali  ya  tahadhari.

Kichwa  cha  habari   katika  ukurasa  wa  mbele  wa  gazeti  rasmi  la  serikali  Rodong Sinmun limeandika  kuhusu  mkutano  kati  ya  Kim  na  Trump  bila  ya  kutaja  ukweli  kwamba  viongozi hao  wawili  wamerejea  nyumbani  mikono  mitupu.

Picha  zimemuonesha  Kim  akizungumza  na  Trump , mtu  ambaye  hapo  zamani alimshambulia  kwa  kusema kuwa  ni  Mmarekani  mlemavu  wa  akili.

"Walikuwa  na  mazungumzo  mazuri  na  walibadilishana  mawazo   kuhusiana  na  masuala halisi  yanayotokana  na  ufunguzi  wa  enzi  mpya  ya kuboresha  uhusiano  kati  ya  Korea kaskazini  na  Marekani  kwa  msingi wa  hatua  zitakazopigwa ," limeandika  gazeti  la  Rodog.

Korea Kaskazini ilitaka maafikiano

Picha: Reuters/L. Millis

Vyombo  vya  habari  vya  taifa  havikueleza  lolote  kuhusiana  na  kushindwa  kwa  mazungumzo ama  kutokubaliana  kuhusiana  na  madai  ya  Korea  kaskazini  ya  kufikishwa  mwisho  vikwazo na  miito  ya  Marekani  ya  kuharibu  kabisa  mpango  wote  wa  kinyuklia  wa  Korea  kaskazini.

Waziri wa mambo ya kigeni wa  Korea kaskazini Ri Yong Ho amesema nchi yake ilitoa mapendekezo halisi katika  mkutano  huo.

Shirika  rasmi  la  habari la Korea kaskazini  pia  lilichukua  msimamo  wa  mapatano  zaidi, likisema  Kim ametoa  shukrani  zake  kwa  Trump  kwa  kuwezesha  juhudi  zenye  manufaa  na kufanikisha  mkutano  huo  na  mazungumzo  wakati  amefanya  safari  ndefu na  kusema  kwaheri, na  kuahidi  mkutano  mwingine.

Vyombo  vya  habari  nchini  Japan  mshirika  wa  Marekani  vililenga hata  hivyo katika  kuvunjika kwa  mazungumzo  hayo  pamoja na  shaka  juu  ya  hali  ya  baadaye  ya  diplomasia  ya  kinyuklia kutokana  na  jinsi  pande  hizo  mbili  zilivyoshindwa  kupunguza  mwanya  licha  ya  uhusika  wa binafsi  wa  viongozi  hao  katika  majadiliano.

Washirika wa Marekani wana wasiwasi

Picha: Reuters/K. Hong-Ji

Wachambuzi  wengi  nchini  Japan, nchi  ambayo  mara  kwa  mara  ni  lengo  la  vitisho  vya Korea  kaskazini , wamekuwa  na  wasi  wasi  kwamba  Trump  anaweza  kufikia  makubaliano ambayo  yataiacha  nchi  hiyo  ambayo  ni  mkoloni  wa  zamani  wa  Korea  kaskazini  ikiwa katika hali  ya  kupewa  vitisho vya  kinyuklia  wakati  wowote.

Rais  wa  Korea  kusini Moon Jae-In  amesema  leo kwamba  serikali  yake  ina  mipango ya kufanya  majadiliano  na  Marekani  kuhusu uwezekano  wa  kuanzisha  miradi  ya pamoja  ya kiuchumi  kati  ya  Korea  kaskazini  na  Korea  kusini kuishawishi  nchi  hiyo  kuachana  na mpango  wa  kinyuklia.

Kim Jong Un ameanza  ziara  rasmi  nchini  Vietnam leo baada  ya  mkutano  wake  na  Trump.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW