1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Korea Kaskazini yakataa kuendelea na mazungumzo na Kusini

28 Julai 2025

Korea Kaskazini imetangaza kulikataa pendekezo la Korea Kusini la kuendeleza mazungumzo ya amani na ushirikiano kati ya mataifa hayo ndugu lakini yaliyohasimiana kwa miongo kadhaa sasa.

Korea Kaskazini Kim Yo Jong
Dada wa kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Yo Jong.Picha: Jorge Silva/AP Photo/picture alliance

Dada wa kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Yo Jong, amesema kwenye taarifa yake kupitia shirika la utangazaji la nchi yake kwamba Korea Kaskazini haina haja ya kuingia kwenye majadiliano na Kusini,licha ya wito wa rais mpya, Lee Jae Myung, ambaye anajaribu kuachana na siasa za uhasama za mtangulizi wake.

Kwenye ripoti iliyotangazwa leo, Kim Yo Jong, ambaye anaaminika kuwa na ushawishi mkubwa kwenye utawala wa kaka yake, Kim Jong Un, amesema Korea Kusini isitegemee kamwe kwa Kaskazini kuvutika na ahadi zake za uongo kuhusu mapatano.

Kim Yo Jong amedai kuwa mahusiano baina ya pande hizo mbili yameshaharibika mno kiasi cha kwamba hayarekebishiki tena.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW