1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaKorea Kusini

Korea Kusini yapanga kuwafidia waganga wa kazi za laazima

6 Machi 2023

Korea Kusini imetangaza mipango ya kuwalipa fidia waathirika wa vitendo vya utumikishwaji kwa nguvu vilivyofanywa na wanajeshi wa Japan wakati wa vita, nchi hiyo ilipoikalia kwa mabavu rasi ya Korea Kusini kwa miaka 35

Südkorea Erster Tag der Unabhängigkeitsbewegung
Picha: Kim Hong-Ji/REUTERS

Hata hivyo waathirika wameukosoa mpango huo kwa sababu haujayafikia mapendekezo yao ya kutaka kuombwa radhi kikamilifu na Japan na kulipwa fidia moja kwa moja na makampuni ya Kijapani yaliyohusika na vitendo hivyo.

Pendekezo hilo lilikaribishwa mjini Tokyo lakini lilikabiliwa na upinzani wa mara moja kutoka kwa baadhi ya waathirika na kutoka chama kikuu cha upinzani cha Korea Kusini, ambao waliishutumu serikali kwa kusalimu amri kwa Japan.

Uamuzi huo wa Seoul umetangazwa wakati Korea Kusini na Japan zinaimarisha ushirikiano wa kiusalama kufutia ongezeko la vitisho kutoka Korea Kaskazini yenye nguvu za Kinyuklia.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW