1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Putin yuko tayari kwa makubaliano ya amani Ukraine

20 Julai 2025

Urusi kupitia msemaji wa Ikulu Dmitry Peskov imesema rais wa nchi hiyo Vladimir Putin yupo tayari kufikia makubaliano ya amani na Ukraine lakini dhamira ya utawala mjini Moscow ni kutimiza malengo yake ya vita.

Moscow |  Vladimir Putin
Rais wa Urusi Vladimir Putin Picha: Mikhail Metzel/Sputnik Kremlin/AP/dpa/picture alliance

Peskov amesisitiza kuwa safari ya kufikia usitishaji wa mapigano Ukraine inahitaji uvumilivu na siyo rahisi. 

Insert Peskov "Rais Putin amerejea kusema mara kadhaa juu ya shauku yake ya kufikisha mwisho mzozo wa Ukraine kwa njia ya amani haraka iwezekanavyo. Huo ni mchakato mrefu na unahitaji juhudi mahsusi na siyo kitu rahisi. Na inaonekana Marekani polepole itakuja kulielewa hili." 

Vikwazo vipya dhidi ya Urusi katika njia panda

Rais wa Marekani Donald Trump amerejelea mara kadhaa matamshi yake ya kutaka kuumaliza mzozo wa Ukraine haraka lakini amesema amevunjwa moyo na tabia isiyotabirika ya rais Putin.

Jumatatu ya wiki hii, Trump alitangaza nia ya kuchukua msimamo mzito dhidi ya Urusi, akiahidi msaada mkubwa zaidi wa kijeshi kwa Ukraine, ikiwemo kuipatia mifumo mambo leo ya ulinzi chapa Patriot. Vilevile aliipatia Urusi muda wa mwisho wa siku 50 kufikia makubaliano ya kusitisha vita au ikabiliwe na vikwazo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW