1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KUALA LUMPUR: Ahadi ya kushirikiana zaidi kiuchumi

25 Julai 2006
Nchi za Asia ya kusini-mashariki katika mkutano wa kilele nchini Malaysia leo hii zimeapa kuharakisha mpango wa kuanzishwa uhusiano wa kiuchumi kati yao.Tangazo hilo limetolewa baada ya mazungumzo ya Shirika la Biashara Duniani-WTO,kuvunjika siku ya jumatatu,mjini Geneva, Uswissi.Kuvunjika kwa mkutano wa WTO umesababisha lawama katika jumuiya ya kimataifa.Mkuu wa biashara wa Umoja wa Ulaya,Peter Mandelson ameituhumu Marekani inayokataa kupunguza ruzuku zinazolipwa kwa wakulima wa Kimarekani na kuathiri biashara duniani.
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW